RESEARCH ARTICLE
descriptionPDFUrasimishaji wa Maneno ya Mkopo kutoka Kiswahili
katikaLugha yaKimalila
Year 2021, Volume: 1, Issue: 1, 185-215, 2021-03-09
Azimio Sote
Ikisiri
Makala haya yamejikita katika kuchambua michakato
inayotumika kurasimisha nomino za mkopo katika lugha ya
Kimalila [M 24] zinazotoka katika lugha ya Kiswahili kwa
kumakinika katika vipengele vya kifonolojia na kimofolojia.
Data za utafiti huu zilikusanywa kwa njia ya hojaji na ushiriki,
ambapo jumla ya maneno 312 yalichunguzwa. Makala
yameonesha kwamba nomino zote zinazokopwa kutoka lugha ya
Kiswahili kwenda lugha ya Kimalila ni lazima ziboreshwe
walau kwa kuwekewa toni na kiambishi awali tanglizi.
Mabadiliko mengine yaliyobainika ni ya udondoshaji na
uchopekaji wa sauti pamoja na uambishaji wa maumbo ngeli
mawili katika shina moja. Maboresho haya yanafanyika ili
yaendane na fonolojia pamoja na mofolojia ya lugha ya
Kimalila. Inaonesha kuwa hakuna neno la mkopo kutoka lugha
ya Kiswahili linalorasimishwa bila kuboreshwa. Hata hivyo,
kuwepo kwa maneno mengi ya Kiswahili katika lugha ya
Kimalila kunaweza kuwa na athari katika uhai wa lugha
Kimalila. Ipo haja ya tafiti zaidi kufanyika kuhusiana na athari
za lugha ya Kiswahili au lugha nyingine katika lugha ya
Kimalila.
Maneno Muhimu
Kiswahili, Kimalila, maneno ya mkopo,
nomino, michakato ya urasimishaji
Details
Primary Language
Kiswahili
Journal Section
Research Article
Publication Date
2021-03-09
Submission Date
0000-00-00
Acceptance Date
0000-00-00
Cite