RUAHA CATHOLIC UNIVERSITY

Ruaha Journal of Arts and Social Sciences (RUJASS)

RESEARCH ARTICLE
descriptionPDF
Kutathmini athari za kimatamshi za kihaya kama lugha ya kwanza kwa wanaojifunza kiswahili sanifu kama lugha ya pili
Year 2024, Volume: 9, Issue: 2, 53-71, 2024-12-29
Godfrey Ndaluhela
Ikisiri
Utafiti huu ulitathmini athari za matamshi za Kihaya kama lugha ya kwaza kwa wanaojifunza Kiswahili sanifu kama lugha ya pili. Wataalamu wengi wanakubaliana kuwa lugha zinapokutana huwa zinaathiriana. Utafiti ulifanyika katika mkoa wa Kagera katika wilaya ya Missenyi, Tanzania. Mbinu zilizotumika kukusanya data ni hojaji na ushuhudiaji. Data za utafiti huu zimechanganuliwa kwa mkabala wa kimaelezo na kuongozwa na Nadharia ya Lugha Kadirifu. Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa, kuna athari za uchopekaji wa fonimu, udondoshaji wa fonimu na kubadilisha fonimu. Aidha, Makala hii imeweka bayana mbinu zinazotumiwa na walimu kuwasaidia wazungumzaji wa Kihaya kujifunza Kiswahili sanifu ambazo ni kusoma kwa sauti, masahihisho kwa fonimu, nyimbo, kurudia rudia kutamka maneno, kutumia vielelezo na michoro na kuwapatia wanafunzi kazi za kutafuta maneno yenye silabi husika.
Maneno Muhimu
Athari za matamshi, lugha ya Kihaya, lugha ya Kiswahili, sanifu
Details

Primary Language
Kiswahili

Subjects

Journal Section
Research Article

Authors
Godfrey Ndaluhela

Publication Date
2024-12-29

Submission Date
2024-10-15

Acceptance Date
2024-02-02

Cite

APA
Godfrey Ndaluhela. (2024). Kutathmini athari za kimatamshi za kihaya kama lugha ya kwanza kwa wanaojifunza kiswahili sanifu kama lugha ya pili. Ruaha Journal of Arts and Social Sciences, 9(2), 53-71.content_copy

Copyright © 2025 RUCU, All Rights Reserved.