RESEARCH ARTICLE
descriptionPDFUbunga Unavyoakisiwa katika Fasihi ya Kiswahili
Year 2021, Volume: 1, Issue: 1, 238-253, 2021-03-09
Gerephace Mwangosi
Ikisiri
Tamthiliya katika jamii na mazingira ya Afrika Mashariki
inatumika kama chombo kinachomudu harakati mbalimbali za
kijamii. Baadhi ya masuala yanayoelezwa ni mwingiliano na
uhusiano wa kisanaa, kimaudhui na kiutamaduni unaoweza
kuthibitishwa kupitia kazi za fasihi ya Kiswahili.Makala haya
yamechunguza nafasi na usawiri wa Ubunga katika fasihi ya
Kiswahili kwa kurejelea tamthiliya teule za Mfalme Juha na
Amezidi. Ubunga katika sanaa unalenga kujenga misingi ya
kuifunza na kuifikirisha jamii kwa kutumia mbinu ya ucheshi na
kusisitiza uwazi kulingana na hali halisi ya uzoefu wa maisha
ya binadamu na mazingira yake.Data za msingi za makala haya
zimepatikana maktabani kwa kudurusu vitabu teule
vilivyobainishwa. Mapitio ya nyaraka zilizotumika kuthibitisha
data za msingi pia zimepatikana kwa mbinu za usomaji wa
nyaraka. Nadharia ya Unafsia imetumika katika uchambuzi na
mjadala wa data zilizowasilishwa.Makala yanahitimisha kuwa
ubunga katika fasihi ni mojawapo ya vyombo muhimu vya
kiharakati vinavyomudu mahitaji ya jamii kwa kuzingatia hali
halisi ya mifumo na mitindo ya maisha ya binadamu.
Maneno Muhimu
Kaida, Ubunga, Muakiso, Unafsia
Details
Primary Language
Kiswahili
Journal Section
Research Article
Authors
Gerephace Mwangosi
Publication Date
2021-03-09
Submission Date
0000-00-00
Acceptance Date
0000-00-00
Cite