RESEARCH ARTICLE
descriptionPDFKategoria ya Vimahali katika Lugha ya Kiswahili
Year 2021, Volume: 1, Issue: 1, 254-278, 2021-03-09
Fabiola Hassan
Ikisiri
Wanaisimu wa lugha ya Kiswahili wameainisha vimahali katika
kategoria ya vielezi. Vimahali vinarejelea mahali tendo
lilipotendeka, linapotendeka au litakapotendeka. Vilevile, ni
vielezi kwa sababu vimeambikwa kiambishi tamati cha mahali
–ni. Hata hivyo, matumizi ya vimahali katika tungo
yanadhihirisha kuwa vina tabia za nomino. Makala haya
yanabainisha kategoria ya vimahali katika Kiswahili kwa
kuzingatia tabia zake za kisemantiki, kimofolojia na sintaksia
kwa kuwa makala haya yanahusisha mofolojia, sintaksia na
semantiki. Data za makala haya zimepatikana kwa mbinu ya
uchambuzi wa matini mbalimbali za Kiswahili pamoja na
upimaji wa usahihi wa kisarufi. Ufafanuzi wa data hizo
umetumia nadharia ya Sampuli Kifani, ambayo inatoa fursa ya
kuzichambua data zinazoonesha mwingiliano wa kikategoria
pamoja na udarajia wa umemba katika kategoria za maneno.
Makala yanabainisha kwamba kategoria ya vimahali
hutegemea sifa za kisemantiki, kimofolojia na matumizi yake
katika tungo. Hitimisho la makala haya ni kwamba vimahali ni
maneno yenye mwingiliano wa kikategoria.
Maneno Muhimu
Vimahali, vielezi, nomino, chagizo, kiima,
yambwa, kijalizo
Details
Primary Language
Kiswahili
Journal Section
Research Article
Publication Date
2021-03-09
Submission Date
0000-00-00
Acceptance Date
0000-00-00
Cite