RUAHA CATHOLIC UNIVERSITY

Jarida la Fahari ya Kiswahili (JAFAKI)

RESEARCH ARTICLE
descriptionPDF
Matumizi ya Lugha Yanavyoibua Dhamira katika Ushairi wa Kiswahili
Year 2022, Volume: 1, Issue: 1, 1-16, 2022-02-10
Charles Mbiu
Ikisiri
Makala hii imechunguza matumizi ya lugha yanavyoibua dhamira katika ushairi wa Kiswahili. Utafiti huu umefanywa kwa kurejelea diwani mbili, yaani Wasakatonge (2003) na Chini ya Mwembe (2017). Data za msingi za makala hii zilipatikana maktabani kwa mbinu ya usomaji makini na uchambuzi wa nyaraka. Matokeo ya utafiti uliozaa makala hii yameonesha jinsi kipengele cha lugha kinavyoibua dhamira katika diwani teule. Vipengele vya lugha vilivyowasilishwa vilikitwa katika mazingira, historia na utamaduni wa jamii iliyomkuza na kumlea mwandishi. Pia, imeonesha kuwa lugha na dhamira ni vipengele vinavyotegemeana na kukamilishana katika kazi ya fasihi. Makala hii inapendekeza kuwa serikali itunge kanuni na sheria kali ili kudhibiti matumizi ya lugha ya fasihi za kigeni zisizoendana na uhalisia wa mazingira ya Tanzania na Afrika kwa ujumla.
Maneno Muhimu
Matumizi ya Lugha, Dhamira na Ushairi wa Kiswahili.
Details

Primary Language
Kiswahili

Subjects

Journal Section
Research Article

Authors
Charles Mbiu

Publication Date
2022-02-10

Submission Date
0000-00-00

Acceptance Date
0000-00-00

Cite

APA
Charles Mbiu. (2022). Matumizi ya Lugha Yanavyoibua Dhamira katika Ushairi wa Kiswahili. Jarida la Fahari ya Kiswahili, 1(1), 1-16.content_copy

Copyright © 2025 RUCU, All Rights Reserved.