RESEARCH ARTICLE
descriptionPDFMuakiso wa Uhalisi wa Kauli za Mhusika Mlevi katika
Fasihi ya Kiswahili
Year 2021, Volume: 1, Issue: 1, 216-237, 2021-03-09
Lazaro Mlelwa
Ikisiri
Tamthiliya ya Kiswahili ni miongoni mwa kazi za kisanaa zenye
wajibu mkubwa wa kuijenga jamii katika hali mbalimbali
kupitia wahusika wake. Kwa kawaida, wahusika hudhibitiwa na
kuathiriwa kwa kiasi kikubwa na muktadha wa utunzi, hasa
mawazo yanayowahusu waandishi kulingana na falsafa zao,
mazingira yao, utamaduni wao, hali ya maisha na harakati
zilizopo katika jamii inayohusika. Makala haya yanachunguza
muakiso wa uhalisi wa kauli za mhusika mlevi katika kazi za
kifasihi. Zaidi pia, kuna urejeleaji watamthiliya teule za Lina
Ubani (1984) na Mabepari wa Bongo (2007). Data za msingi
za makala haya zimepatikana maktabani kwa kudurusu
tamthiliya teule zilizobainishwa. Mapitio ya nyaraka
zilizotumika kuthibitisha data za msingi pia zimepatikana kwa
mbinu za usomaji wa nyaraka. Uchambuzi na mjadala wa data
zilizowasilishwa umeongozwa na nadharia ya Ucheshi. Makala
haya yanahitimisha kuwa mhusika mlevi ni mojawapo ya
mawakala wa kazi za kifasihi kwa kuwa huyafichua na
kuyaweka wazi mambo yote yanayoshindikana kusemwa na
wahusika wakiwa katika ungāamuzi tambuzi.
Maneno Muhimu
Muakiso, Mlevi, Mhusika, Ucheshi,
Tamthiliya ya Kiswahili
Details
Primary Language
Kiswahili
Journal Section
Research Article
Publication Date
2021-03-09
Submission Date
0000-00-00
Acceptance Date
0000-00-00
Cite