RUAHA CATHOLIC UNIVERSITY

Jarida la Fahari ya Kiswahili (JAFAKI)

RESEARCH ARTICLE
descriptionPDF
Utata katika Ufasiri wa Maana za Sitiari za Kiswahili
Year 2022, Volume: 1, Issue: 1, 77-91, 2022-02-10
Mofart Onyoni Ayiega
Ikisiri
Makala hii imechunguza utata katika ufasiri wa maana za sitiari za Kiswahili. Data ya makala hii ilisakurwa mtandaoni kutoka kwa tafiti za awali, majarida na makala kwa kuongozwa na sampuli lengwa. Data ilikusanywa kwa kutumia mbinu ya usomaji makini. Ili kubaini utambuzi wa msikilizaji na msomaji ujumbe, mtafiti aliwaomba wazungumzaji 12 wa Kiswahili kufasiri maana ya sitiari husika kwa kuongozwa na maswali ya mahojiano huru. Nadharia ya Semantiki Tambuzi ilitumiwa katika uchambuzi wa data ya utafiti huu. Matokeo ya utafiti huu yalibaini kuwa utata katika ufasiri wa maana za sitiari za Kiswahili husababishwa na tajriba na maarifa ya mpokeaji ujumbe, muktadha wa matumizi ya sitiari, elimu, taswira na mazingira ya mpokeaji ujumbe. Pia, makala hii yameeleza namna uhamishaji wa maana hutokea katika uundaji wa maana katika sitiari inayohusika. Uchunguzi huu ulitambua kuwa hakuna maana mahsusi ya sitiari kwa kuwa maana zake huwa ni dhana zilizo akilini mwa binadamu. Makala hii inapendekeza kwamba ni vyema sitiari kufasiriwa bila kujikita katika maana moja.
Maneno Muhimu
Sitiari, utata, semantiki, isimu tambuzi na uhamishaji maana
Details

Primary Language
Kiswahili

Subjects

Journal Section
Research Article

Authors
Mofart Onyoni Ayiega

Publication Date
2022-02-10

Submission Date
0000-00-00

Acceptance Date
0000-00-00

Cite

APA
Mofart Onyoni Ayiega. (2022). Utata katika Ufasiri wa Maana za Sitiari za Kiswahili. Jarida la Fahari ya Kiswahili, 1(1), 77-91.content_copy

Copyright © 2025 RUCU, All Rights Reserved.