RUAHA CATHOLIC UNIVERSITY

Jarida la Fahari ya Kiswahili (JAFAKI)

RESEARCH ARTICLE
descriptionPDF
Mapungufu ya Kiutamaduni Yanavyoathiri Ustawi wa Mwanamke katika Jamii: Mifano Kutoka Riwaya ya Sikujua
Year 2022, Volume: 1, Issue: 1, 115-300, 2022-02-10
Ndimyake Mwakanjuki
Ikisiri
Makala hii imechunguza mapungufu ya kiutamaduni yanavyoathiri ustawi wa mwanamke katika jamii kwa kurejelea riwaya ya Sikujua. Data za msingi zilipatikana katika riwaya ya Sikujua kwa mbinu ya usomaji makini. Mbinu ya uteuzi lengwa ilitumika kupata riwaya teule. Data za upili kwa ajili ya kufafanua na kuthibitisha data za msingi zilipatikana kwa mbinu ya usomaji wa nyaraka mbalimbali. Makala yamebainisha kuwa utamaduni ni asasi mojawapo ya iliyosheheni taarifa na sheria zilizoeleza uhusiano usio sawa baina ya mwanamke na mwanamke katika jamii. Mwanamke amekuwa mhanga wa kasoro zinazoendelea kumdhalilisha na kumdunisha mwanamke. Makala haya yanapendekeza kuwa jamii haina budi kubadilika kwa kuacha utamaduni unaomdhulumu mwanamke. Serikali na taasisi zisizo za kiserikali zinapaswa kuendelea kukemea kisheria hali yoyote inayonuia kumdhalilisha mwanamke kwa kurejelea misingi ya mila na desturi zilizopo katika jamii.
Maneno Muhimu
Mapungufu, Utamaduni, Mwanamke, Riwaya na Ufeministi
Details

Primary Language
Kiswahili

Subjects

Journal Section
Research Article

Authors
Ndimyake Mwakanjuki

Publication Date
2022-02-10

Submission Date
0000-00-00

Acceptance Date
0000-00-00

Cite

APA
Ndimyake Mwakanjuki. (2022). Mapungufu ya Kiutamaduni Yanavyoathiri Ustawi wa Mwanamke katika Jamii: Mifano Kutoka Riwaya ya Sikujua. Jarida la Fahari ya Kiswahili, 1(1), 115-300.content_copy

Copyright © 2025 RUCU, All Rights Reserved.