RUAHA CATHOLIC UNIVERSITY

Jarida la Fahari ya Kiswahili (JAFAKI)

RESEARCH ARTICLE
descriptionPDF
Nyimbo za Asili Zinavyoimarisha Mafunzo ya Jadi nchini Tanzania
Year 2022, Volume: 1, Issue: 1, 34-53, 2022-02-10
Deus Gracewell Seif
Ikisiri
Makala hii imechunguza dhamira za nyimbo za Wakaguru katika kujenga na kuimarisha mafunzo ya jadi nchini Tanzania. Data za msingi za makala hii zilikusanywa uwandani kwa kutumia mbinu za mahojiano na usaili. Utafiti ulifanyika uwandani katika mkoa wa Morogoro, wilaya ya Gairo. Utafiti uliozaa makala hii umebaini kuwa dhamira za nyimbo za Wakaguru hutumiwa kama ghala maalumu lililosheheni taarifa na maarifa yaliyopo katika jamii. Nyimbo hizo zinasaidia kuifunza jamii masuala ya utamaduni, siasa na uchumi wa jamii hiyo kutoka kizazi kimoja hadi kizazi kingine. Misingi ya mila, desturi, falsafa, historia na maendeleo yao yanarejelewa katika vipengele vingi vya maisha yao ya jadi. Pia, hutumika kama kiungo thabiti cha kiasili kinachojenga mfumo wa kuifunza, kuiimarisha na kuiweka jamii pamoja katika misingi ya utamaduni na falsafa nzima ya maisha tangu kale mpaka sasa. Makala hii inapendekeza kuwa ufundishwaji wa fasihi za jadi utolewe na taasisi husika na zifanyiwe tarijama kwa ajili ya vizazi vilivyopo na vijavyo. Pia, serikali itunge kanuni kali za kudhibiti matumizi ya fasihi za kigeni zisizoendana na uhalisi wa mazingira ya kiasili, zikiwemo kanda za picha za utupu.
Maneno Muhimu
Nyimbo za kiasili, nyimbo za Wakaguru na mafunzo ya Jadi.
Details

Primary Language
Kiswahili

Subjects

Journal Section
Research Article

Authors
Deus Gracewell Seif

Publication Date
2022-02-10

Submission Date
0000-00-00

Acceptance Date
0000-00-00

Cite

APA
Deus Gracewell Seif. (2022). Nyimbo za Asili Zinavyoimarisha Mafunzo ya Jadi nchini Tanzania. Jarida la Fahari ya Kiswahili, 1(1), 34-53.content_copy

Copyright © 2025 RUCU, All Rights Reserved.