RUAHA CATHOLIC UNIVERSITY

Ruaha Journal of Arts and Social Sciences (RUJASS)

RESEARCH ARTICLE
descriptionPDF
Matumizi ya Tanakali Sauti katika Nyimbo/Misemo/Masimulizi ya Matambiko ya Jamii ya Wabena Nchini Tanzania
Year 2024, Volume: 9, Issue: 1, 77-89, 2024-02-02
Leopard Jacob Mwalongo
Ikisiri
Makala hii inahusu uchunguzi wa matumizi ya tanakali sauti kwenye matambiko ya jamii ya Wabena mkoani Njombe nchini Tanzania. Data za msingi zilizotumika katika makala hii zilipatikana kwa mbinu ya mahojiano na usaili katika wilaya ya Njombe Mjini na Njombe Vijijini, mkoani Njombe. Kijiji cha Luponde na Lusitu (Kata ya Luponde) Ihalula na Lugenge (Kata ya Utalingoro) ndivyo vilivyolengwa katika wilaya ya Njombe Vijijinii. Kwa upande wa Njombe Mjini, vijiji vilivyolengwa ni Mjimwema na Joshoni (Kata ya Mjimwema) Idundilanga na Ramadhani (Kata ya Njombe mjini.). Uchambuzi wa data uliongozwa na nadharia ya Uhalisiajabu. Makala hii imebaini kuwa matambiko ya jamii ya Wabena yamesheheni matumizi ya tanakali sauti ambazo zinatumika kwa malengo mbalimbali yakiwemo yanayohusu kuweka msisitizo na kusawiri uhalisi wa jambo fulani katika jamii ya Wabena. Pia, yamebaini kwamba matambiko yana namna tofauti tofauti za matumizi ya vipengele vya lugha lengo maalumu kwa kurejelea muktadha mahususi wa tambiko teule. Makala hii inapendekeza utafiti zaidi juu ya matumizi ya lugha katika matambiko mbalimbali ndani na hata nje ya nchi.
Maneno Muhimu
Matambiko, Jamii ya Wabena, Tanakali Sauti na Nadharia ya Uhalisiajabu
Details

Primary Language
Kiswahili

Subjects

Journal Section
Research Article

Authors
Leopard Jacob Mwalongo

Publication Date
2024-02-02

Submission Date
0000-00-00

Acceptance Date
0000-00-00

Cite

APA
Leopard Jacob Mwalongo. (2024). Matumizi ya Tanakali Sauti katika Nyimbo/Misemo/Masimulizi ya Matambiko ya Jamii ya Wabena Nchini Tanzania. Ruaha Journal of Arts and Social Sciences, 9(1), 77-89.content_copy

Copyright © 2025 RUCU, All Rights Reserved.