RESEARCH ARTICLE
descriptionPDFMatumizi ya Lugha Hasi Yanavyoathiri Malezi ya Watoto, Ujifunzaji na Mustakabali
wa Maisha Yao
Year 2024, Volume: 3, Issue: 2, 59-76, 2024-12-02
Rose Sekile, Sebastian Nyerere Mbwillow
Ikisiri
Makala haya yanahusu matumizi ya lugha katika malezi yanavyoathiri ujifunzaji na mustakabali
wa maisha yao. Kimsingi, makala yanalenga kujadili matumizi ya lugha hasi katika malezi na
tendo zima la ujifunzaji. Aidha, makala yanalenga kuielekeza jamii jinsi lugha ilivyo na
mchango mkubwa wa kuweza kujenga utu na kumuandaa mtu bora, au mbaya, kuzindua fikra za
wanajamii ili wawe na mtazamo chanya kuhusu matumizi lugha wakati wa kulea watoto. Data
zilizofanikisha makala haya zilitokana na utafiti wa uwandani kwa kiasi kikubwa na kimaktaba
kwa kiasi kidogo. Data za msingi zilipatikana katika jamii. Data hizi zilipatikana kwa wazazi,
walimu na wanafunzi walioko shule za msingi, sekondari, na vyuo. Mbinu ya usomaji makini na
upembuzi yakinifu zilitumika kupata data za msingi. Nadharia iliyoongoza uchanganuzi wa data
ni Nadharia ya Ethnografia ya Mawasiliano ya Dell Hymes (1974). Makala haya yanaonesha
kuwa lugha hasi zimekuwa zikizungumzwa katika miktadha mbalimbali kama nyumbani,
kwenye elimu, na katika jamii. Fauka ya hayo, matumizi ya lugha hasi katika miktadha tajwa
huacha athari hasi kwa watoto hasa kisaikolojia. Makala haya yanahitimisha kwa kuitaka jamii
iwe na uelewa mpana kuhusu matumizi ya lugha wakati wa malezi, kwa sababu lugha
inayotumika inaweza kuwaathiri watoto. Watoto ni sehemu kubwa ya jamii, na ndiyo tegemeo
la uendelevu wa taifa lolote, hivyo hatuna budi kuwalea vizuri na kuwaendeleza ili waweze
kutimiza ndoto zao.
Maneno Muhimu
Lugha, Malezi, Ujifunzaji, Mustakabali
Details
Primary Language
Kiswahili
Journal Section
Research Article
Authors
Rose Sekile, Sebastian Nyerere Mbwillow
Publication Date
2024-12-02
Submission Date
0000-00-00
Acceptance Date
0000-00-00
Cite