RUAHA CATHOLIC UNIVERSITY

Jarida la Fahari ya Kiswahili (JAFAKI)

RESEARCH ARTICLE
descriptionPDF
Ufutuhi kama Mbinu ya Kuwasilisha Dhamira za Kisiasa katika Katuni za Mtandaoni za Masoud Kipanya
Year 2022, Volume: 1, Issue: 1, 54-65, 2022-02-10
Majuto Kapaya Manyuka
Ikisiri
Makala hii inashughulikia ufutuhi katika katuni za kisiasa za Masoud Kipanya. Kilichochunguzwa hapa ni mbinu za ufutuhi katika katuni za kisiasa na namna zinavyowasilisha mawazo ya kisiasa katika jamii ya Tanzania. Data za msingi zilikusanywa maktabani kwa mbinu ya uchanganuzi matini wa katuni zilizochapishwa katika akaunti ya Masoud Kipanya katika mtandao wa kijamii wa Instagram. Data za upili kwa ajili ya ufafanuzi wa data za msingi zilipatikana kwa mbinu ya usomaji wa nyaraka. Nadharia ya Semiotiki imetumika ili kufasili ishara za katuni na mawazo ya kisiasa yanayowasilishwa na mbinu za ufutuhi. Makala hii imebainisha kuwa katuni za kisiasa za Kipanya hutumia mbinu za ufutuhi katika kujadili na kuwasilisha mawazo mbalimbali ya kisiasa. Mbinu za ufutuhi ni muhimu katika kuwasilisha ujumbe uliokusudiwa. Makala hii inapendekeza kufanyika kwa tafiti zaidi kuhusu ufutuhi katika tanzu mbalimbali za fasihi.
Maneno Muhimu
Ufutuhi, mbinu za ufutuhi, katuni, katuni za kisiasa na mtandaoni
Details

Primary Language
Kiswahili

Subjects

Journal Section
Research Article

Authors
Majuto Kapaya Manyuka

Publication Date
2022-02-10

Submission Date
0000-00-00

Acceptance Date
0000-00-00

Cite

APA
Majuto Kapaya Manyuka. (2022). Ufutuhi kama Mbinu ya Kuwasilisha Dhamira za Kisiasa katika Katuni za Mtandaoni za Masoud Kipanya. Jarida la Fahari ya Kiswahili, 1(1), 54-65.content_copy

Copyright © 2025 RUCU, All Rights Reserved.