RUAHA CATHOLIC UNIVERSITY

Jarida la Fahari ya Kiswahili (JAFAKI)

RESEARCH ARTICLE
descriptionPDF
Utandawazi wa Kiswahili: Kuimarika na Kulegalega kama Lugha Rasmi ya Afrika
Year 2022, Volume: 1, Issue: 1, 105-114, 2022-02-10
Mohamed Omary Maguo
Ikisiri
Makala hii imechunguza utandawazi wa Kiswahili, kuimarika na kulegalega kwake kama lugha rasmi ya Afrika. Data za msingi katika makala hii zilipatikana maktabani kwa kudurusu nyaraka zinazohusiana na mada teule. Data za upili zilizotumika kuthibitisha data za msingi zilipatikana maktabani kwa mbinu ya usomaji makini. Matokeo ya utafiti uliozaa makala hii yameonesha historia, maendeleo na kuimarika kwa utandawazi wa Kiswahili Barani Afrika. Pia, imeonesha sababu za kihistoria, kisera na kisaikolojia zinazosababisha kulegalega kwa Kiswahili kama lugha rasmi ya Afrika. Baadhi ya mataifa yanadai kuwa lugha za kikoloni ni vigezo muhimu vya kupima hadhi ya taifa kiuchumi, kisayansi na kiteknolojia. Muelekeo huu unaangukia katika kuzienzi lugha za Kikoloni na unaambatana na jitihada za kupuuza lugha za asili za Kiafrika kwa kuziona katika uchanga usioweza kumudu mahitaji ya utandawazi. Makala hii inapendekeza kuwa ni wakati muafaka kwa mataifa ya Afrika kuunda sera ya lugha itakayohusisha mataifa yote na itakayotekeleza kwa vitendo. Kwa kufanya hivyo, lugha ya Kiswahili itakuwa alama ya Uafrika na lugha rasmi ya Afrika.
Maneno Muhimu
Utandawazi, Kiswahili, lugha rasmi, kuimarika na kulegalega
Details

Primary Language
Kiswahili

Subjects

Journal Section
Research Article

Authors
Mohamed Omary Maguo

Publication Date
2022-02-10

Submission Date
0000-00-00

Acceptance Date
0000-00-00

Cite

APA
Mohamed Omary Maguo. (2022). Utandawazi wa Kiswahili: Kuimarika na Kulegalega kama Lugha Rasmi ya Afrika. Jarida la Fahari ya Kiswahili, 1(1), 105-114.content_copy

Copyright © 2025 RUCU, All Rights Reserved.